AHAZI

AHAZI

Monday, July 25, 2016

Cheka kidogo

*SOMA HII NA CHEKA KWA KUONGEZA AFYA.*
*Mwelevu na Mjinga walienda ktk usaili, walipofika kabla hawajaingia wakakubaliana aanze Mwerevu kisha akitoka ampe majibu Mjinga ili wote wapate kazi.*

*Basi Mwerevu akaingia na maswali yakawa hivi:-*
*Msaili:- Tanzania ilipata Uhuru mwaka gani?*

*Mwerevu:- ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mpaka 1961 kutokana na sababu mbalimbali..*

*Msaili:- Nani hasa alihusika na upatikanaji wa Uhuru huo?*

*Mwerevu:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J.K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia.*

*Msaili:- Inasemekana katika sayari ya Mars kuna viumbe wanaishi, je ni Kweli?*

*Mwerevu:- Watu wengi wanasema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.*

*Baada ya Mwerevu kutoka basi Mjinga akapewa majibu yote..*

*Kuingia ktk usaili maswali yakawa hivi:-*

*Msaili:- Tuambie ulizaliwa mwaka gani?*

*Mjinga:- Ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mbele mpaka mwaka 1961 kutokana na sababu mbali mbali.*

*Msaili:- Mungu Wangu, BABA yako anaitwa nani?*

*Mjinga:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J. K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia .*

*Msaili:- Hivi wewe ni chizi?*

*Mjinga:- watu wengi husema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi*😂😂😂



aPosted via Blogaway

No comments:

Post a Comment