AHAZI

AHAZI

Sunday, July 31, 2016

Bustan

JINSI YA KUTENGENEZA BUSTANI NDOGO YA NYUMBANI
Kuna njia mbali mbali waweza kuepuka kutumia mboga mboga zinazolimwa usikokujua na kuepuka kujiingiza katika afya mbaya kwa matumizi ya kemikali za kuulia wadudu na magonjwa zinazotumika katika ukuzaji wa mboga mboga.

Aina za bustani
1. Unaweza tumia makopo amabayo mara nyingi hutumika kupanda maua kando kando ya nyumba
2. Unaweza tumia gunia la sandarusi kubwa..
3. Unaweza tengeneza key hole garden ( bustani ya tundu la Ufunguo)

Bustani Ya Makopo/Ndoo

Vifaa
Udongo, makopo/ndoo, mchanga/Pumba za mpunga (Rice husk), Mbole ya samadi iliooza vizuri.
Udongo - Kwa ajili ya kuwezesha mmea kusimama, pia kupatia virutubisho mmea

Mchanga/Rice husk - Kusaidia mizizi kupita kwa urahisi, pia kuweka mazingira mazuri ya hewa na maji katika udongo yaani mzunguko wa maji na hewa. 

Mbolea ya samadi - Kutoa virutubisho kwa mmea

Hatua za utengenezaji.
- Changanya udongo wako na mchanga/rice husk pamoja na mbole katika uwiano wa 5:2:1.
   5 udongo, 2 samadi, 1 Mchanga/rice husk
- Toboa makopo yako kwa chini ili kuzuia maji kubaki kwa wingi kwenye kupo na weka pamba kwenye matundu uliotoboa.
- Weka udongo uliochanganywa vizur kwenye makapo/ndoo. Hapo utakuwa tayar kupanda mbegu zako ama mche wa mboga aina yoyote.
- Kuepuka uchafuzi wa mazingira kwa maji yanayo toka kwenye makopo endapo makopo hayo yapo kwene simenti, weka makopo/ndoo hayo juu sahani/besen

Uangalizi.
- Mwagilia mboga yako mara tu baada ya kupanda na kuendelea ikitegemeana ni aina gani ya mboga.
- Unapoona magonjwa hasa fangasi wa ukungu na wadudu wa mboga unaweza tumia dawa zisizo za kemikali za viwandani kama vile  majani ya pilipili kichaa, mwarobaini na tumbaku.
- Mboga kama sukuma wiki waweza vuna mara kwa mara, kazi yako ni kumwagilia tu.
- unatakiwa kubadilisha udongo wako kwa muda mfano. baada ya mavuno 2 ili kuakikisha mboga zako zina pata virutubisho ya kutosha.. ( Hii inategemeana ni aina gani ya mboga)

Faidi
- Inapunguza utumiaji wa kemikali za viwandani
- Gharama za uhitaji wa mboga za majani.

SEHEMU YA PILI YA UTENGENEZAI WA BUSTANI NDOGO ZA NYUMBANI
BUSTANI YA GUNIA
Vifaa
Udongo, Kokoto (mawe madogo madogo), Gunia, mchanga/Pumba za mpunga (Rice husk), Mbole ya samadi iliooza vizuri, mti/mbao na kopo dogo (sadolini).
Udongo - Kwa ajili ya kuwezesha mmea kusimama, pia kupatia virutubisho mmea
Mchanga/Rice husk - Kusaidia mizizi kupita kwa urahisi, pia kuweka mazingira mazuri ya hewa na maji katika udongo yaani mzunguko wa maji na hewa. 
Kokoto  - Kusadia maji kupita ndani ya gunia toka juu hadi chini
Mbolea ya samadi - Kutoa virutubisho kwa mmea
mti/Mbao  - Kusaidia gunia lako kusimama vyema/ imara

Hatua za utengenezaji.
  (i)   Changanya udongo wako na mchanga/rice husk pamoja na mbole katika uwiano wa 5:2:1.
         5 udongo, 2 samadi, 1 Mchanga/rice husk.
(ii)    Toboa kopo lako na ondoa kitako ili kuweka uwazi pande zote mbili (juu na chini)
(iii)  Weka mti/ubao katikati ya gunia ukiuchimbia ardhini kisha weka kopo lako katikati ya mti/mbao hiyo na lijaze kokoto 

(iv)  Weka udongo uliochanganywa vizur kwenye gunia lako ukilizunguka kopo lenye kokoto hadi kufikia kimo cha kopo. Baada ya hapo ondoa kopo na hakikisha kokoto zinabaki zikizungukwa na udongo.
(v)  Weka kopo juu ya kokoto zilizozungukwa na udongo kisha, lijaze kopo hilo na kokoto, rudia kujaza udongo ukilizunguka kopo hadi kimo cha kopo hilo. Endelea kufanya hivyo (kama hapo juu) hadi pale gunia lako litakapokuwa limejaa.
(vi) Toboa gunia kwa kuweka matundu kuzunguka gunia kwa ajili ya kupandia katika umbali sawa (inategemea na aina ya mboga)

(vii) Hapo utakuwa tayari kupanda mbegu zako ama mche wa mboga aina yoyote juu na pembeni ya gunia lako


Mboga aina ya letuce (Lactuca sativa)

Mboga aina ya sukumawiki (Brassica carinata) zikiwa zimepandwa kwenye gunia

Uangalizi.
- Mwagilia mboga yako mara baada tu ya kupanda na kuendelea ikitegemeana ni aina gani ya mboga.
- Unapoona magonjwa hasa fangasi wa ukungu na wadudu wa mboga unaweza tumia dawa zisizo za kikemikali za viwandani kama vile  majani ya pilipili kichaa, mwarobaini na tumbaku.
- Mboga kama sukuma wiki waweza vuna mara kwa mara, kazi yako ni kumwagilia tu.
- unatakiwa kubadilisha udongo wako kwa muda mfano. baada ya mavuno 2 ili kuakikisha mboga zako zina pata virutubisho ya kutosha.. ( Hii inategemeana ni aina gani ya mboga)
Muhimu: Ukitumia miche kwa siku tatu/mbili za mwanzo usije ogopa kuona miche yako imelala endelea kuimwagilia itasimama tu. Pia katika umwagiliaji hakikisha unamwaga maji katika kati ya guni pale kulipo na kokoto ili kuhakikisha maji yanasamba ndani ya gunia hadi chini.
Faidi
- Inapunguza utumiaji wa kemikali za viwandani
- Gharama za uhitaji wa mboga za majani.
- inatumia nafasi ndogo na kutoa kiasi kikubwa cha  mboga mboga.



aPosted via Blogaway

Bustani popote

*BUSTANI YA MFUKO/GUNIA*

               *Mahitaji*

1. Chukua mfuko, gunia au salfate,

2. Andaa udongo, mchanga na mbolea kwa ratio ya 1:1:1

3. Andaa kokoto.

4. Kopo kisadolin hawa kikiwa kile chenye mfumo wa pipa ili kiwe na kipenyo sawa pande zote then litoboe hilo kopo liwe waz pande zote

*Utengeneza*

*i* Changanya mchanganyiko wa udongo, mbolea na mchanga

*ii* chukua mfuko wako ufunue uwe wazi ikibid uukunje ili kimo kipungue kidogo

*iii* weka kopo lako ktkt ya mfuko lijaze kokoto hilo kipo

*iv* weka udongo wako uliouandaa kwenye mfuko had kufikia kimo cha kopo lako.

*v* livute juu hilo kopo ili kokoto zibak livute had lifikie usawa wa juu zilipoishia kokoto zako za kwanza

*rudia kuweka kokoto, na udongo kama (iii) na (iv) alafu then namba (v) had ufikie juu usawa wa mfuko wako.*

VI. Toboa mfuko kwa umbal wa cm15 kati ya shimo na na shimo kama unapanda chines, sukumawik na mimea inayofanana na hiyo.

*bustan ya mfuko inafaa kupanda mboga mboga na ni rahisi kuhudumia*

*Note* unapoweka udongo hakikisha unashindilie ili utakapomwagia maji mfuko usijikunje

*unapomwagilia maji mimina kwenye kokoto na udongo wote utapata maji*



aPosted via Blogaway

Hii dawa hatari

KINYWAJI KITACHOFANYA UONE TUMBO LIKIPOTEA NDANI YA WIKI MOJA
Chukua jagi kubwa na weka vifuatavyo:
1. Maji na slice za:
2. Matango yaliyokatwakatwa
3. Malimao au Ndimu
4. Mdalasini
5. Tangawizi au Manjano ukiweza kupata
6. Majani ya mint (ukipata)

Weka mchanganyiko kwenye friji na tumia kama maji ya kawaida. Ukipenda maji yakiisha weka maji mapya, ila ni vizuri zaidi ukila hayo matunda na kuweka mengine fresh. Ukiachana na kuondoa mafuta ya tumbo, mchanganyiko huu ni mzuri kwa kuondoa sumu mwilini. Kama ladha unaiona kali sana, ruksa kuongeza kijiko cha asali. Share na wengine wajifunze!



aPosted via Blogaway

Dawa za kuku

Madawa ya Asilihbxx  c yatokanayo na Mimea yanayosaidia katika Tiba na Kinga za Maradhi mbalimbali ya Kuku💫

A.  Sehemu za mimea zinaweza kuwa: Majani, Magome, Mbegu, Maua au Matunda

B.  Umuhimu wa kutumia tiba zenye asili ya mimea:

•  Hupatikana kwa urahisi.
•  Ni rahisi kutumia.
•  Gharama nafuu.
•  Zinatibu vizuri.
•  Hazina madhara.

C.  Baadhi ya Mimea inayotibu Maradhi ya Kuku:

1.  Mwarobaini (Majani, Mizizi, Magome):
Hutibu magonjwa yafuatayo:
•  Typhoid.
•  Kuzuia Kideri.
•  Kuhara.
•  Mafua.
•  Vidonda.

2.  Shubiri Mwitu (Aloe vera):
Chukua majani 3-5 makubwa, katakata na loweka ndani ya maji lita 10 kwa masaa 12 hadi 16. Wape kuku kwa siku 5 - 7.
Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine baada ya masaa 12.

Mchanganyiko huu unaweza kutibu:
•  Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba/Kitoga/Chinoya/Sotoka)
- inyweshwe kabla kwa kinga.
•  Homa ya matumbo (Typhoid).
•  Mafua (Coryza).
•  Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera).

3. Mtakalang’onyo (Euphorbia):

Chukua Majani makubwa 3-5, ponda, weka katika lita 10 za maji kwa masaa 12-16, chuja na wape kuku. Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine.

Mtakalang’onyo hutibu:
•  Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba) - inyweshwe kabla kuzuia
•  Gumboro.
•  Ndui.
•  Kuhara damu (Coccidiosis).

4.  Mbarika (Nyonyo):
Hutibu Uvimbe.

Weka majani ya mbarika ndani ya majani ya mgomba kisha weka ndani ya jivu la moto, kisha kanda sehemu yenye uvimbe kwa kutumia majani hayo ya mbarika.

5.  Mlonge (Mlonje):
Ina vitamini A na C.

Chukua majani ujazo wa mikono miwili (gao mbili). Kisha yapondeponde na kuyaweka katika lita 10 za maji na iache kwa masaa 12-16, chuja na wape kuku. Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine.

Mlonge hutibu:
•  Mafua.
•  Kideri - inyweshwe kabla kwa kukinga
•  Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera).
•  Homa ya matumbo
•  Ini.

6.  Konfrei:
•  Ina madini na vitamini nyingi.
•  Hutibu vidonda na majipu.

7.  Ndulele (Dungurusi, Makonde, Tura/Ndula):
•  Majani hutibu Minyoo.
•  Matunda hutibu Vidonda.

8.  Papai (Majani):
Chemsha magao mawili ndani ya maji lita 6 hadi ubakie na lita 1. Poza kisha chuja.
Hutibu: Minyoo

9.  Mwembe:
Majani magao mawili, ponda na chemsha ndani ya lita 6 za maji hadi ibaki lita 1. Wape kwa siku moja.

Mwembe hutibu:
•  Homa ya matumbo.
•  Mafua.
•  Kinga ya Kideri/Mdondo.

10. Mpira:
Chemsha majani au mizizi.

Mpira hutibu:
•  Tumbo
•  Vidonda na majipu

11.  Minyaa (Cactus):
Hii ni aina yenye majani manene-hadi kufikia nusu nchi na mapana hadi kufikia upana wa viganja viwili vya mikono.

Minyaa hutibu: (Angalia inaunguza au kubabua).
•  Vidonda.
•  Ngozi.
•  Uzazi.

12. Pilipili Kichaa:
Pondaponda kiasi kisha changanya na maji na wawekee kuku wawe wanakunywa kwa muda wao. Inasemekana inasaidia kutibu Mdonde (lakini mapema kabla maradhi kuingia).



aPosted via Blogaway

Monday, July 25, 2016

Cheka kidogo

*SOMA HII NA CHEKA KWA KUONGEZA AFYA.*
*Mwelevu na Mjinga walienda ktk usaili, walipofika kabla hawajaingia wakakubaliana aanze Mwerevu kisha akitoka ampe majibu Mjinga ili wote wapate kazi.*

*Basi Mwerevu akaingia na maswali yakawa hivi:-*
*Msaili:- Tanzania ilipata Uhuru mwaka gani?*

*Mwerevu:- ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mpaka 1961 kutokana na sababu mbalimbali..*

*Msaili:- Nani hasa alihusika na upatikanaji wa Uhuru huo?*

*Mwerevu:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J.K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia.*

*Msaili:- Inasemekana katika sayari ya Mars kuna viumbe wanaishi, je ni Kweli?*

*Mwerevu:- Watu wengi wanasema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.*

*Baada ya Mwerevu kutoka basi Mjinga akapewa majibu yote..*

*Kuingia ktk usaili maswali yakawa hivi:-*

*Msaili:- Tuambie ulizaliwa mwaka gani?*

*Mjinga:- Ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mbele mpaka mwaka 1961 kutokana na sababu mbali mbali.*

*Msaili:- Mungu Wangu, BABA yako anaitwa nani?*

*Mjinga:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J. K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia .*

*Msaili:- Hivi wewe ni chizi?*

*Mjinga:- watu wengi husema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi*😂😂😂



aPosted via Blogaway

Thursday, July 21, 2016

Jamii moja nchini Malawi Jamaa analipwa ili kuwatoa mabinti wa kike usichana

MIX Jamii moja nchini Malawi Jamaa analipwa ili kuwatoa mabinti wa kike usichana By Newsroom TZA
onJuly 21, 2016 9SHARES COMMENTS

Habari hii imeripotiwa na BBC Swahili kuhusu jamii moja nchini Malawi ambayo haithamini ubikira wa watoto wao wa kike. BBC Swahili wameripoti kuwa katika jamii hiyo wazazi wanamlipa mwanaume kumbikiri binti yao punde tu anapopata hedhi yake ya kwanza.

Jamii hiyo inaamini kwamba kuwa na binti ambaye ni bikira ni mkosi kwa jamii, wazazi na jamii kwa ujumla katika maeneo mengi ya kusini mwa Malawi wamekuwa wakishikilia tamaduni hii kwa miaka na miaka.



Wanaume wanaowabikiri watoto wa kike huchaguliwa na wazazi kuwaondolea mikosi, na huwa ni sherehe kubwa inayomtangulia binti kupelekwa unyagoni kisha kuwatembelea shangazi wake kabla ya kujulishwa kwa ‘fisi’.

Mafisi hulipwa takriban dola 7 ambayo ni kama Tsh 15,324 kwa kila kitendo cha ngono na hao mabinti ambao wengi huwa na kati ya umri wa miaka 11-14. Fisi mmoja katika kijiji cha Nsanje, Eric Aniva ameiambia BBC kuwa hajui kwa kweli amewabikiri wasichana wangapi……

>>>”kwa kweli mimi nimewabikiri zaidi ya wasichana 104, hiyo ndio tamaduni zetu pia hapa mwanamke akifiwa lazima aje kwangu nimuondolee mkosi hata kabla ya kuzikwa kwa mumewe’‘.



Aniva ambaye ana umri wa takriban miaka 40 ana wanawake wawili na watoto 5, anasema kuwa pale anaposhiriki ngono na watoto hao huwa anapewa muda wa siku 3 hivi kumsafisha na kumuondolea mkosi.Kulingana na tamaduni zao, ikiwa mwanamke au binti anakataa asibikiriwe huwa wanaamini kuwa jamaa zao watafuatwa na mikosi na magonjwa.



aPosted via Blogaway

Friday, July 15, 2016

Ufugaji kuku

LEO TUANGALIE MCHANGANUO WA TSHS 300,000/= (LAKI TATU) KWA KUANZISHA MTADI WA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI.
Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanao taga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu 300 au na zaidi kama unataka.
Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.
Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.
Usinunue kuku kabla hujaandaa banda na Chakula.
Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.
Mchanganuo Wa 69500 ni:-
Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.
- paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.
-mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500
- layer's consetraite
Kilo 25 kifuko. = 21500.
Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.
Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.
Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku
Hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300.
Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.
TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.
Mchanganuo wake
Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.
Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500
-Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wakutaga
Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.
Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.
Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.
Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200. Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe. Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.
Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote.



aPosted via Blogaway

Thursday, July 7, 2016

Wednesday, July 6, 2016

Bibi yangu kizaa babu

Skanege  bibi kizaa babu  angindikike  mzaa baba john



aPosted via Blogaway

Sunday, July 3, 2016

Maharagwe ya nazi



MAHARAGE YA NAZI

Maharage kikombe kidogo 1 ya kawaida au yanaozwa kwenye kikopo
Nyanya ya kopo nusu au robo kikombe (Tomato sause/purée)
Chumvi kiasi
Thomu kijiko cha chai 1
Tangawizi  kijiko cha chai 1
Nazi ya kopo kibati kimoja au unaweza ukakuna nazi ukawa na tui zito
Pilipili boga kiasi
Kitunguu maji kiasi
Mafuta ya kupikia kiasi

**Chemsha maharage yako yakishaiva yamwage maji au Kama maharage ya kopo mwaga maji na uweke pembeni**
**Weka mafuta ya kupikia kwenye sufuria lako na ukaange kitunguu maji, pilipili boga, tangawizi na thomu***
**Vikishaiva weka nyanya yako ya kopo ikaange kidogo Kisha weka maharage**
**Yaache maharage Kama dakika mbili, Kisha weka nazi yako na usisahau kuweka Chumvi**
**Epua maharage yako nazi ikiiva, usiache yakauke sana**



aPosted via Blogaway